Friday, 6 March 2015

Chuo kikuu cha Moi chaonyesha umahiri kwenye maonyesho



Chuo kikuu cha moi kimeonyesha umahiri wake katika maonyesho ya kilimo mwaka huu mjini Eldoret baada ya kuzoa jumla ya vikombe vitano.
Chuo hiki kimeorodheshwa kuwa chuo bora katika masomo ya kiwango cha juu, chuo bora katika uhandisi, chuo bora katika utafiti, chuo bora kitechnolojia na chuo bora kilichokuwa na chandarua chema katika maonyesho hayo.

Aidha, chuo kiliorodheshwa kuwa chuo cha pili bora baada ya chuo kuku cha Eldoret katika kuekeza technologia mpya.
Rais wa taifa Mheshimiwa Uhuru Muigai Kenyatta anatarajiwa kuhutubia wananchi katika maonyesho hayo hii leo


No comments:

Post a Comment