Viongozi wa TSA
wamelalamikia vikali kutengwa
kwao na muungano wanafunzi wa MUSO
pamoja afisi kuu za utawala za hapa chuoni.
Akiongea na wanahabari aliyekuwa mwenyekiti wa TSA bwana Fredrick Orem amesema
kuwa afisi za utawala zimekuwa zikiwanyima wanafunzi wa shule teknolojia haki yao ya kidemokrasia kwani kila mipango
ya kuwachagua viongozi wa wanafunzi inaporatibiwa basi wanafunzi wa TSA huwa
hawapo shuleni.
Orem aliongezea kuwa chama cha MUSO pia kimekuwa kikiwatenga
TSA katika kupanga miradi inayowahusu wanafunzi wote kwa jumla.
Aidha Orem alijiweka wazi na kusema kuwa yupo tayari kushirikiana na mwenyekiti
na viongozi wateuliwa wote ili kuwasilisha lalamiko lao kwa afisi kuu za
utawala wa humu chuoni.
Yamkini umebobea kwenye lugha zote mbili kwa uandishi.
ReplyDeleteshukrani sana..
Delete